![]() |
Mkaa ukiwa unasafirishwa toka eneo moja kwenda jingine |
Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe amepiga marufuku usafirishaji wa mkaa nje ya wilaya iliyouzalisha.
Ametoa tamko hilo alipokuwa akifungua mkutano wa tano wa Baraza la Wafanyakazi la wakala wa Huduma za Misitu(TFS) mjini Dodoma.
“Kuanzia sasa kibali cha kukata miti kwa ajili ya mkaaa kitolewe na
kusimamia kuwa mkaa unaokatwa na kuchomwa ndani ya wilaya utumike ndani
ya wilaya hiyo tu! Hakuna kusafirisha nje ya wilaya, agizo hili lianze
kutekekelezwa kuanzia Leo tarehe 28/02/2017," amesema Mhe. Magembe.
Katika harakati za kupamabana na biashara ya usafirishaji mkaa, Mhe. Maghembe ameagiza Wakuu wa Wilaya kurudishwa katika Kamati za Uvunaji za Wilaya zenye jukumu la kugawa mazao ya misitu kwa kuzingatia Mpango wa Uvunaji ulioandaliwa na Afisa Misitu na Meneja wa Misitu wa wilaya husika.
Katika harakati za kupamabana na biashara ya usafirishaji mkaa, Mhe. Maghembe ameagiza Wakuu wa Wilaya kurudishwa katika Kamati za Uvunaji za Wilaya zenye jukumu la kugawa mazao ya misitu kwa kuzingatia Mpango wa Uvunaji ulioandaliwa na Afisa Misitu na Meneja wa Misitu wa wilaya husika.
0 comments:
Post a Comment