Shamba la Miti Kawetire lipo
katika Wilaya ya Mbeya Vijijini Mkoani Mbeya, ndani ya msitu wa hifadhi ya
Usafwa kaskazini na Safu ya mlima Mbeya. Shamba lipo kilimita 12 kutoka Mbeya
mjini katika barabara kuu ya Mbeya – Chunya.
Shamba lilianzishwa mwaka 1937 na
serikali ya kikoloni kwa madhumuni ya uzalishaji wa kuni kwa ajili ya migodi ya
dhahabu ya Chunya.
Ili kutimiza azma hiyo miti jamii ya
mikaratusi ilipandwa katika eneo la Ipinda. Upanuzi ulifanyika mwaka 1942, 1950
na 1974 kwa kupanda miti jamii ya misindano (Pinus spp) na mikambokambo (Cupressus
lusitanica) na kulifanya shamba lililopandwa kufikia ukubwa kama ilivyo
sasa.
Baada ya uhuru madhumuni ya mashamba ya
miti likiwemo la Kawetire yaliboreshwa kwenda sambamba na Sera ya misitu
ambayo ni;
- Kuhakikisha upatikanaji endelevu wa mazao na huduma za misitu kwa kuwa na maeneo ya kutosha na yenye usimamizi madhubuti.
- Kupanua ajira na kuongeza pato la fedha kutokana na maendeleo endelevu katika viwanda vinavyojikita kwenye misitu.
- Kuimarisha mifumo ikolojia kwa kuhifadhi bioanuwai ya misitu maeneo ya lindimaji na rutuba ya udongo.
- Kukuza uwezo wa taifa katika kusimamia na kuendeleza sekta ya misitu kwa kushirikiana na washikadau wengine.
Eneo
la Shamba la Miti Kawetire lina msimu mmoja wa mvua ambapo huanza kunyesha
mwezi Novemba na kuendelea hadi mwezi April mwaka unaofuata
Mtiririko unaonesha kwamba miezi ya Juni na Oktoba ni mikavu na kati ya Juni na Agosti ni kipindi cha baridi kali na mara nyingine hali ya joto hufikia nyuzi -5 ̊C hasa wakati wa usiku.
Mtiririko unaonesha kwamba miezi ya Juni na Oktoba ni mikavu na kati ya Juni na Agosti ni kipindi cha baridi kali na mara nyingine hali ya joto hufikia nyuzi -5 ̊C hasa wakati wa usiku.
Kwenye miezi ya joto ya Oktoba na Novemba kiasi cha joto hufikia nyuzi joto 35 ̊C.
Shamba la miti kawetire lina ukubwa wa hecta 5,280 ambazo zimegawanyika kama ifuatavyo ;
Eneo lililopandwa miti limeongezeka kutoka hekta 1,563 mwaka 2012/2013 hadi hekta 2,720 mwaka 2015/2016 hii inamaanisha upandaji umefanywa katika maeneo mapya kwa ukubwa wa hekta 1,157 kuanzia mwaka 2012/2013 hadi 2015/2016.
Maelezo ya maeneo
|
Hekta
|
Eneo lililopandwa miti (mpaka 2012)
|
1,563
|
Eneo la upanuzi lililopandwa miti
2012/2013 – 2015/2016
|
1,157
|
Jumla la eneo lilipandwa miti
|
2,720
|
Eneo la upanuzi ambao halijapandwa
miti(makadirio)
|
471
|
Jumla kuu
|
3,191
|
Eneo la msitu wa asili ni hekta 1,572
na eneo hili limejumuisha maeneo yenye vyanzo vya maji.
Kwa ajili ya usimamizi shamba limegawanywa
katika sehemu sita zinazojulikana kama Safu. Shamba hili linaongozwa na Meneja
wa shamba ambaye anawajibika kwa Mtendaji Mkuu Wakala wa Huduma za Misistu
Tanzania (TFS).Meneja wa Shamba ana meneja msaidizi. Safu husimamiwa na wakuu
wa safu.Hawa pamoja na wakuu wa vitengo mbalimbali kama vile Uvunaji na leseni,
Miundombinu, Ulinzi wa msitu na Nyuki,Uhasibu na Ugavi huwajibika kwa meneja wa
Shamba.
Shamba lina watumishi wa kudumu 34 wa
kada mbalimbali na watumishi wa mkataba 9, Maafisa misitu (4), Wasaidizi Misitu
wa Stashahada na Astashahada (7), Wasaidizi Misitu (20), Mhasibu (1), Katibu
Muhtasi (1) na Tabibu (1).Aidha kutokana na ufinyu wa watumishi tuna watumishi
wanaofanya kazi kwa mkataba wa mwaka mmoja mmoja ambao ni madereva (2), Walinzi
(6), Fundi bomba (1).
Shamba lina mpango wa Usimamizi
(Management Plan) wa kipindi cha miaka mitano.Mpango huo wa usimamizi ndio
mwongozo wa kuendesha Shamba na kuandaa mipango kazi na bajeti za kila mwaka (Annual
Plan of Operations). Mpango wa usimamizi wa sasa ulianza 2012/2013 hadi
2017/2018.
Mpango huu unahusisha kazi zifuatazo
- · Kazi za shambani (Ukuzaji wa miche ya miti katika bustani iliyopo Kawetire na Mbeya Peak) kuandaa mashamba kwa ajili ya upandaji miti katika maeneo yaliyovunwa na katika maeneo ya upanuzi (Extension area), Upandaji miti,usafi wa mashamba (sanitary slashing), kupogoa matawi, doria kwa ajili ya ulinzi wa msitu,ujenzi na ukarabati wa barabara za msituni na uvunaji miti.
- Kazi za utawala na mafunzo (Mikutano, Mafunzo ya muda mfupi, safari za kikazi, likizo za watumishi, ujenzi na ukarabati wa majengo na nyumba za kuishi watumishi, uendeshaji wa magari,manunuzi mbalimbali na kazi za utawala kwa ujumla)
Katika mwaka wa fedha 2012/2013 Jumla
ya hekta 275 zilipandwa kwenye maeneo ya upanuzi na hekta 95 kwenye maeneo
yaliyovunwa miti.Hii inafanya jumla ya eneo lililopandwa kwa mwaka huo kuwa
hekta 370.
Katika mwaka wa fedha 2013/2014 Jumla
ya hekta 165 zilipandwa katika maeneo ya upanuzi katika Safu ya Lwanjiro na
Ipinda na hekta 129 zilipandwa katika maeneo yaliyovunwa katika safu za
Kawetire na Ipinda.
Kwa kipindi cha miaka mitatu ya fedha
tumekuwa tukivuka lengo la upandaji kwani katika mwaka wa fedha 2012/2013
upandaji ulikuwa 149%. Kwa mwaka wa fedha 2013/2014 upandaji ulikuwa 156.5% na
2014/2015 upandaji ulikuwa 112% haya ni mafanikio makubwa kwa shamba na Wakala
kwa ujumla.
Changamoto iliyopo ni kuhakikisha
kwamba nguvu na gharama kubwa iliyotumika kwa ajili ya upandaji miti
haipotei.Tumeweka mikakati ya kuhakikisha miti inatunzwa kwa uangalizi wa hali
ya juu ikiwa ni pamoja na kuhakikisha tunafanya usimamizi wa karibu ili
kuilinda miti.
Shamba la miti kawetire tumekuwa
tukikusanya maduhuri ya serikali yanayotokana na uuzaji wa miti
ambapo mwenendo wa ukusanyaji maduhuri ni kama
ifuatavyo.
FY
|
Volume
|
TOTAL
|
2012/13
|
6,867
|
344,968,053
|
2013/14
|
17,636
|
823,327,314
|
2014/15
|
17,737
|
882,335,080
|
2015/16
|
12,168
|
498,150,755
|
TOTAL
|
54,408
|
2,548,781,202
|
Katika shamba la miti Kawetire tumeanzisha
mradi wa ufugaji nyuki na hadi sasa tuna mizinga ipatayo 100 kati ya hiyo
mizinga yenye nyuki kwa sasa ni 31.
Katika taarifa za miaka iliyopita moja
kati ya changamoto ambazo zimekuwa zikionekana kwenye taarifa hizo ni uchakavu
wa nyumba za watumishi, na baadhi ya nyumba hizo zilijengwa mwaka 1937,
kimsingi nyumba ni chakavu na nyingi zinahitaji kubomolewa kwani hazifai tena
kufanyiwa ukarabati.Kwa nyumba ambazo zina unafuu wa kufanyia ukarabati,
tumefanikiwa kufanya ukarabati mkubwa na mdogo pamoja na ujenzi wa vyoo.
Ukarabati huu unaendelea kufanyika kadri bajeti inavyoruhusu. Hii ni katika
kuhakikisha kwamba watumishi wanaishi katika mazingira ya kuridhisha na masafi.
Pamoja na shughuli za upandaji miti na
shughuli mbalimbali shamba linawezesha na kutoa huduma mbalimbali kwa jamii
inayozunguka shamba na taifa kwa ujumla.Uwezeshaji na huduma hizi ni kama
ifuatavyo;
Shamba linaajiri vibarua wa kutwa zaidi
ya 600 kwa mwaka kwa ajili ya kutekeleza shughuli mbalimbali za shamba, vibarua
wengi huajiriwa wakati wa upandaji miti, kutengeneza barabara za moto na ulinzi
wa misitu; wengi wa vibarua ni wenyeji wa mbeya kutoka vijiji vinavyozunguka
shamba.
Wafanyakazi wa shamba na wanavijiji
hugawiwa maeneo ya kulima katika maeneo yaliyovunwa miti. Wastani wa watu 300
hufaidika na huduma hiyo ambayo utaratibu huu hutoa mchango kwenye usalama wa
chakula (food security) na kuongezea wananchi mapato.
Wananchi waishio jirani na shamba
huruhusiwa kuokota kuni kavu kwa ajili ya matumizi ya nyumbani. Wananchi
wanaruhusiwa pia kutafuta mboga katika maneo ya msitu.
Shamba la Miti Kawetire linatoa mchango
katika huduma za afya na maendeleo ya wananchi kwa ujumla. Kuna zahanati moja
ambayo hutoa huduma ya matibabu kwa wanavijiji na watumishi wa shamba. Zahanati
hii imekuwa na mchango mkubwa katika kuhakikisha huduma za afya za watumishi na
wanavijiji wa jirani zinaimarika kwa kutoa elimu juu ya lishe bora na elimu ya
kuzuia maambukizi mapya ya virusi vya ukimwi (VVU).
Shamba pia linachangia katika sekta ya
ujenzi kutokana na mauzo ya miti ambayo inachanwa mbao zinazotumika
kwenye ujenzi.
Katika kuunga mkono agizo la Mh. Raisi
wa Jamhuri ya Mungao wa Tanzania kwamba lazima kila mtoto akalie dawati Shamba
la Miti Kawetire limeanza kutengeneza madawati 264 ambayo yatagawanywa katika
Shule mbalimbali za Wilaya ya Mbeya.
Changamoto mbalimbali zinazolikabili
shamba ambazo ni pamoja na:-
Kusitishwa kwa upandaji wa eneo la
upanuzi safu ya Karuwe
Eneo hili lilikuwa ndani hifadhi yam
situ wa safu ya mlima mbeya lenye ukubwa wa hekta 1280. Eneo hili likuwa
linavamiwa na wananchi mara kwa mara na kufanywa eneo la malisho, kilimo
na uwindaji hivyo kupelekea matumizi ya moto wakati wakiendesha shughuli zao na
kusababisha mioto ya mara kwa mara na hivyo kuharibu uoto uliokuwepo.
Kutokana na sababu hiyo eneo hilo
lilihamishwa kutoka kwenye usimamizi wa Kanda na kuhamishiwa kwa Shamba la Miti
Kawetire kwa ajili ya kupanda miti ili kurudishia uoto uliokuwepo, hii ilikuwa
ni pamoja na kupanda miti ya kibiashara na kuhakikisha kwamba Sheria ya
mazingira inafuatwa kwa kuacha vyanzo vya maji umbali wa mita 60 au zaidi.
Upandaji huu ulizingatia kwamba, maeneo
yaliyo mbali na vyanzo vya maji yapandwe miti ya kibiashara na yale yaliyo
karibu na vyanzo vya maji yapandwe miti rafiki ifaayo maeneo hayo ikiwamo na
utunzaji vyanzo hivyo.
Upandaji ulianza Januari 2016 na baada
ya kupanda hekta 295 kati ya 478 zilizotakiwa kupandwa 2015/2016, tulipata zuio
kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya kwamba tusiendelea kupanda wala kuhudumia
miti iliyokwishapandwa kwani kulikuwa na malalamiko kutoka Mamlaka ya maji safi
na usafi wa mazingira ya jiji la Mbeya kwamba tunaharibu vyanzo vya maji.
Shamba la miti kawetire hupata matukio
ya moto ambao kwa kiasi kikubwa husababishwa na shughuli zinazofanywa na
wananchi wanaozunguka msitu kama vile uwindaji, uandaaji wa mashamba na kurina
asali. Matukio haya hupunguza jitihada za usimamizi endelevu wa shamba.
Katika kukabiliana na changamoto hii
uongozi wa shamba la miti kawetire umekuwa ukifanya yafuatayo;
Kuelimisha jamii
- Vijiji kumi na sita vinavyozunguka Shamba hupewa elimu ya kuzuia na kupambana na moto kwa njia ya mikutano ya kampeni ya kudhibiti moto
- Kikosi maalumu cha kupambana na moto kinachofanya kazi saa 24 kwa siku kwa kipindi chote cha kiangazi
- Kutengeneza barabara za kinga dhidi ya moto kuzunguka shamba lote kila mwaka
- Kuchoma barabara za moto wakati ambapo nyasi hazijakauka sana ili kupunguza kasi ya moto pale unapotokea.
- Kuweka ratiba kwa watumishi wote wa shamba kuwa tayari kupambana na moto pale unapotokea.
Shamba halina lori wala “tractor” kwa
ajili ya kusaidia shughuli za bustani na upandaji jambo ambalo linafanya
usafirishaji wa miche kwenda maeneo ya upandaji kuwa mgumu na kuchukua muda
mrefu kwani wakati mwingine tunalazimika kutumia “L/c hardtop”
Ili kukabiliana na changamoto hii,
katika mwaka wa fedha 2015/2016 shamba lilitenga bajeti kwa ajili ya kununua
grader na tractor na mchakato wa manunuzi unaendelea na unafanyika na TFS HQ
Shamba lina upungufu wa watumishi wa
kada mbalimbali hasa madereva na walinzi.
Ili kukabiliana na changamoto hii
shamba huajiri vibarua kwa mkataba wakati tukisubiri ajira za kudumu kutoka
Serikalini.
Majengo na nyumba za watumishi
zimechakaa kwani nyingi zimejengwa mwaka 1937.Nyumba nyingine hazifai hata
kufanyiwa ukarabati kwani zimeanza kubomoka na kuta kuanza kudondoka.
Katika kukabiliana na changamoto hii
pamoja na ufinyu wa bajeti Shamba limeweza kufanya ukarabati mkubwa wa majengo
mawili ,nyumba ishirini na mbili za watumishi, ujenzi wa vyoo, majiko na ujenzi
wa nyumba mbili za watumishi hii imepelekea kubadilisha muonekano wa mandhari
ya nyumba na ofisi.
Eneo la msitu wa nishati wa mbeya
(Mbeya fuel wood) lililokuwa na zaidi ya hekta 300 limekuwa likivamiwa na
kupimwa viwanja na mpaka sasa eneo lililobaki ni kama hekta 67 tu.
Katika kukabiliana na changamoto hii na
kulinusuru eneo lilobaki uongozi wa Shamba umelipima eneo kwa kushirikiana na
Ofisi ya Kanda ya Nyanda za juu Kusini na Halmashauri ya jiji la Mbeya katika
kuandaa mpango kabambe ili kuinua utalii wa Mikoa ya Nyanda za juu Kusini. Kazi
hii inaendelea na ipo katika hatua ya upimaji na upangaji wa viwanja kwa ajili
ya makazi, mahoteli, nyumba za ibada, viwanja vya michezo na maeneo yatakayo
hifadhiwa.
0 comments:
Post a Comment