 |
Kaimu
Mtendaji Mkuu Wakala wa Huduma za Misitu nchini, Dos Santos Silayo
(mwenye suti nyeusi) akijadiliana jambo na watendaji wa TFS na
Mkurugenzi wa Mfuko wa Hifadhi ya Wanyamapori na Mazingira Duniani(WWF)
Msumbiji, Bi. Anabela Rodriques (mwenye miwani) kabla ya kuanza kwa
zoezi la kusaini hati ya makubaliano kati ya Serikali ya Tanzania na
Msumbiji, jijini Maputo jana kwa ajili ya kukabiliana na changamoto za
udhibiti wa usafirishaji wa mazao ya misitu hususan mbao katika mipaka
ya nchi hizo mbili. Wengine ni Mkurugenzi wa Mipango na Matumizi ya
Rasilimali wa Wakala wa Misitu nchini Bw. Mohamed Kilongo (mwenye suti)
na mwakilishi wa WWF Tanzania, Bw. Geofrey Mwanjelwa. |
 |
Kaimu
Mtendaji Mkuu Wakala wa Huduma za Misitu nchini, Dos Santos Silayo
(mwenye suti nyeusi) akisaini kusaini hati ya makubaliano kati ya
Serikali ya Tanzania na Msumbiji, jijini Maputo jana kwa ajili ya
kukabiliana na changamoto za udhibiti wa usafirishaji wa mazao ya misitu
hususan mbao katika mipaka ya nchi hizo mbili. Wengine ni Katibu Mkuu
wa Wizara ya Ardhi Mazingira na Maendeleo Vijijini, Bi. Sheila Afonso
pamoja na mtendaji wa Wizara hiyo (hakuweza kufahamika jina lake mara
moja). |
Serikali kupitia Wakala wa Huduma za Misitu nchini imefanya mazungumzo
na kusaini hati ya makubaliano na Serikali ya Msumbiji kupitia Wizara ya
Ardhi Mazingira na Maendeleo Vijijini mjini Maputo Msumbiji jana
kuthibiti uvunaji na usafirishaji wa mazao ya misitu katika maeneo
mipaka ya nchi hizi mbili.
Akisaini makubaliano hayo
yaliyoratibiwa na Mfuko wa Hifadhi ya Wanyamapori na Mazingira
Duniani(WWF)kupitia mradi wa Crossboaders, Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala
wa Huduma za Misitu, Prof. Dos Santos Silayo alisema makubaliano hayo
yatasaidia kukabiliana na changamoto za udhibiti wa usafirishaji wa
mazao ya misitu hususan mbao katika mipaka ya nchi hizo mbili.
“Makubaliano haya kati ya Tanzania na Msumbiji yatasaidia kupiga vita
biashara haramu ya mbao pamoja na mazao ya misitu inayofanyika kupitia
mipaka ya nchi hizi, biashara ya uzalishaji na usafirishaji wa bidhaa za
misitu baina ya nchi hizi umekuwa na tija kutokana na kukua kwa soko la
nyumba. Hivyo kwa pamoja tukishirikiana tutaweza kuhakikisha sheria,
taratibu na kanuni za uzalishaji na usafirishaji wa mazao ya misitu
zinafuatwa,” alisema.
Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara ya
Ardhi Mazingira na Maendeleo Vijijini, Sheila Afonso alipongeza hatua
hiyo muhimu iliyofikiwa na kuahidi kuwa Tanzania itaendelea kuwa rafiki
na ndugu wa dhati wa Msumbiji kama ambavyo mahusiano ya nchi hizi mbili
yamejengwa tangu zamani.
0 comments:
Post a Comment